Ads 468x60px

Labels

Tags

Nature

Comments

Custom Widget

Main Slider

Recent in Sports

Recent

Monday 2 February 2015

FAHAMU MADHARA YA UTAPIAMLO KWA WATOTO.



      Utapiamlo ni ugonjwa unaoathiri kukua kwa mwili na akili ya mtoto. Idadi ya watoto wanaopata ugonjwa huo hapa nchini inakadiriwa kuwa asilimia 42 huku ikiwa inahofiwa kuongezeka ambapo mara nyingi huwapata watoto wenye umri chini ya miaka 18. 

Kwa nini ni vigumu sana kushinda tatizo hilo? Ili kupata jibu, ni vyema kuujuwa kwanza ugonjwa wa utapiamlo, na kuchunguza athari na visababishi vilivyotia mizizi vya ugonjwa huo.

UTAPIAMLO HUSABABISHWA NA NINI?
Utapiamlo husababishwa na ukosefu wa vitamini na madini ya kutosha katika chembe za mwili, na kwa kawaida husababishwa na mambo mawili:



  •  Ukosefu wa protini, nishati, vitamini, na madini.

  • Maambukizo ya mara kwa mara.


Magonjwa kama vile kuharisha, surua, malaria, na magonjwa ya kupumua hudhoofisha mwili sana na kupunguza vitamini na madini. Magonjwa hayo humfanya mgonjwa apoteze hamu ya kula naye hula chakula kidogo sana, na hivyo anapata utapiamlo. Kwa upande mwingine, mtoto asiyepata chakula cha kutosha anaweza kuambukizwa magonjwa kwa urahisi. Jambo hilo huongeza idadi ya watoto wanaokufa kwa sababu ya kukosa vyakula vinavyojenga mwili.

KWA NINI UTAPIAMLO UNAWASHAMBULIA ZAIDI WATOTO ?
Watoto wanakua haraka na hivyo wanahitaji nishati na protini nyingi zaidi. Vivyo hivyo, akina mama wajawazito na wanaonyonyesha wanaweza kupata utapiamlo.

Mara nyingi, mtoto mchanga huanza kuathiriwa akiwa tumboni. Ikiwa mama hapati chakula cha kutosha au hali chakula bora kabla na wakati wa mimba, basi atajifungua mtoto mwenye uzito kidogo. Mtoto huyo akiachishwa kunyonya mapema, asipolishwa vizuri, au usafi usipozingatiwa, anaweza kuugua utapiamlo.

Mtoto hawezi kukua au kusitawi vizuri asipopata vitamini na madini muhimu. Yeye hulia bila sababu yoyote na kuwa mgonjwa-mgonjwa. Kadiri hali yake inavyozorota ndivyo anavyozidi kukonda, macho na utosi wa kichwa hubonyea, ngozi na tishu za mwili hukauka, na uwezo wa kudhibiti joto la mwili hupungua.

Utapiamlo humwathiri mtoto kwa njia nyingine ambazo pia zinaweza kuathiri ukuzi wake. Kwa mfano, kutopata madini ya kutosha hasa chuma, iodini, na zinki na vitamini hasa vitamini A - kunaweza kusababisha madhara hayo. 

MADHARA MABAYA ZAIDI
Utapiamlo hudhuru kabisa mwili, hasa mwili wa mtoto. Unaweza kudhuru viungo na mifumo yote mwilini kutia ndani moyo, mafigo, tumbo, matumbo, mapafu, na ubongo.

Uchunguzi mbalimbali umeonyesha kwamba ukuzi wa polepole wa mtoto hudhoofisha maendeleo yake ya kiakili na uwezo wa kufikiri na kufanya vyema shuleni.

Mtoto anaweza kuendelea kuathiriwa na matokeo ya utapiamlo hata anapokuwa mtu mzima.


VISABABISHI
Kama ilivyotajwa awali, utapiamlo husababishwa na ukosefu wa chakula. Lakini, unasababishwa pia na mambo mengine mazito zaidi ya kijamii, kiuchumi, kitamaduni, na ya kimazingira. Kisababishi kikuu ni umaskini, ambao huathiri mamilioni ya watu, hasa katika nchi zinazoendelea. Hata hivyo, mbali na kuwa kisababishi, umaskini pia husababishwa na utapiamlo. Ukosefu wa chakula cha kutosha hupunguza uwezo wa kufanya kazi, na hilo huzidisha umaskini.


KUTIBU NA KUZUIA
Mtoto mwenye utapiamlo anaweza kutibiwaje?
Ikiwa mtoto huyo amedhoofika kabisa huenda ikafaa alazwe hospitalini kwanza

Katika hatua ya pili, mtoto hunyonyeshwa na kusaidiwa ale chakula kingi iwezekanavyo. Ni muhimu kuboresha tena hali yake ya kihisia na ya kimwili wakati huo. Mtoto huyo anaweza kukua vyema akitunzwa kwa uangalifu na kuonyeshwa upendo. Wakati huo huenda ikafaa kumfundisha mama kumtunza mtoto wake kwa kumlisha chakula kinachofaa na kutunza afya yake ili asipate tena utapiamlo. Kisha mtoto hurudishwa nyumbani. Ni muhimu mtoto apelekwe hospitalini au kwenye kliniki ili maendeleo yake yachunguzwe.

Hata hivyo, kuuzuia utapiamlo ndilo jambo la maana zaidi. Ndiyo sababu serikali na mashirika yasiyo ya kiserikali katika nchi nyingi yameanzisha miradi ya kuboresha chakula kinacholiwa na umma. Jamii pia hujitahidi kuzuia utapiamlo kwa njia nyingi, kama vile kuanzisha mipango ya kuwaelimisha watu kuhusu chakula, kuwa na maji safi ya kunywa, kujenga vyoo, kudumisha usafi wa mazingira, kutoa michango kwa ajili ya kampeni za chanjo, na kusimamia ukuzi na maendeleo ya watoto.

Lakini mtu mmoja-mmoja anaweza kufanya nini ili kuzuia utapiamlo Lakini pia mama anashauriwa kirudi hospitali kumwona tena daktari wa watoto au kurudi hospitalini siku saba baada ya kujifungua, mtoto anapokuwa na umri wa mwezi mmoja, na kila mwezi baada ya hapo. Mama anapaswa pia kumwona daktari mtoto anapokuwa na dalili za kupungukiwa na maji mwilini, anaharisha sana, au akiwa na dalili za homa.

                                                                                                                     Posted by Jovith Novath

No comments:

 

Total Pageviews

Blog Archive